Monday, August 19, 2013

AUNT EZEKIEL APASULIWA

Na Imelda Mtema
MKALI wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel amefanyiwa oparesheni ya haraka kwa ajili ya kuondolewa uvimbe tumboni.
Kwa mujibu wa mtu wa karibu na staa huyo, Aunt alikuwa akitembea na uvimbe huo siku nyingi pasipo kujijua hadi alipougua ghafla wakiwa katika mizunguko ya kila siku jijini Dar, mwishoni mwa wiki iliyopita.
“Ghafla alibadilika, hakuwa katika hali ya kawaida kwani tulikuwa tukipiga stori lakini nikashangaa mwenzangu anabadilika kama mtu aliyepandwa na presha hivi.
“Tulilazimika kuahirisha misele yetu, ikabidi twende Hospitali ya Aga Khan na ndipo alipogundulika kuwa ana uvimbe tumboni kisha kufanyiwa upasuaji haraka sana kwani ulikuwa katika hatua mbaya za kuleta madhara,” kilisema chanzo hicho.
Hata hivyo mtu huyo wa karibu ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, alisema staa huyo anaendelea vizuri. 

0 comments:

Post a Comment